Mheshimiwa Paul Makonda Aenda Mbali Zaidi Kutekeleza Alichokiahidi BAKWATA

Kauli ya ufafanuzi ya Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir, kwa Waislam juu ya ujenzi wa jengo jipya la BAKWATA jijini Dar es Salaam.

Kauli ya ufafanuzi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda, kwa Watanzania kwa ujumla juu ya ujenzi wa jengo jipya la BAKWATA jijini Dar es Salaam.

KWA UFUPI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul Makonda, katika hotuba yake ya siku ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la BAKWATA jijini Dar es Salaam, amelenga kusisitiza mchango mkubwa unaofanywa na viongozi wa dini katika nchi yetu, basi haina budi kuwawekea mazingira mazuri ili waweze kutekeleza kazi zao vyema katika jamii, na akasisitiza kwa kusema ataendelea kushirikiana kwa kuwasaidia viongozi wa dini bila ya kusikiliza yanayosemwa vipembeni.

Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir, katika hotuba yake ya siku ya kuwekwa jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la BAKWATA jijini Dar es Salaam, amelenga kusisitiza kwa Waislamu wote kuwa wamoja na kushikamana katika mambo yanayoleta tija zenye faida katika Uislam na akatolea mifano mbalimbali ambayo inawafik hoja ya ujenzi huo kwa dalili za aya za Qur’an na Hadith za Mtume Muhammad (S.A.W) na kuhimiza Waislam wasikae pembeni bali wawe mbele kwenye kutekeleza kwenye mambo ya kuujenga Uislam na siyo kukaa vipembeni na kuonyesha vidole. Mufti Mkuu Sheikh Abubakar Zubeir amesisitiza, pamoja na kuwa kuna baadhi ya watu wana shaka na mchango huo kutolewa kwa njia moja au nyingine na mtu ambaye si Muislam, Mufti Mkuu amewatoa khofu Waislam na wasiokuwa Waislam kwamba mchango huo unafaa baada ya kuangalia pande zote za Sharia, na amegusia kwamba Mheshimiwa Paul Makonda ana nafasi kubwa katika jamii yetu basi si vibaya ikiwa atajitolea mchango wake popote pale anapoona ana uwezo napo kwa nafasi yake. Na mheshimiwa Makonda alisadikisha hilo.

MWISHO WA UFUPI

Kwa kumalizia, hakuna kitu ambacho kikatokea chenye ikhtilaf baina ya mwanadamu kwa mwanadamu, au ikhtilaf baina ya watu mbalimbali wa itikadi zozote zile bila ya kuwa na suluhisho la watu kukaa pamoja na kuheshimiana tofauti zao na kutatua matatizo yao kwenye kila maeneo ya kimaisha.

Na mahsusi kwa hili suala la jengo la BAKWATA kwa maneno yaliyojitokeza kutoka kwa baadhi ya watu kuwa na dhana mbaya kwa viongozi wetu wa dini, hatuna budi tuwakumbushe kwamba Qur’an tukufu inatufundisha kihikma kwamba tunaweza kushirikiana pamoja ili kujenga lengo lolote tarajiwa, mfano Biashara, Amani, Upendo katika jamii na vyote vyenye kumpendeza Mwenyezi Mungu katika mambo mbalimbali ya kimaisha kwa kushirikiana pamoja lakini bila ya kuvuka mipaka ya kiitikadi, iwe ya kisiasa au ya kidini. Pamoja inawezekana bila ya kuvuka mipaka ya Mwenyezi Mungu.

Mbali na kisiasa au kiserikali, iwapo Waislam wanaohoji au watakaohoji hoja ya ushirikiano wa hili (jengo) lenye kuhusu kidini, waangalie Qur’an inavyosema:

Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu.

Qur’an (3:64)

Kwa hili la kidini, tunaishukuru serikali kwa kupitia uongozi wa Mheshimiwa Paul Makonda kwa kutimiza wajibu wake kihekima na kikatiba. Kuna tofauti kubwa baina ya elimu na hekima, elimu huja kwa njia zote za kusoma, za kuona, za kuhisi na za kusikia, lakini hekima ni kufanya maamuzi sahihi ya hali halisi ilivyo kwa kusikiliza hoja za pande zote kwa umakini na kuleta tija kwa lengo tarajiwa na hata mara nyingine mpaka matokeo yake kupelekea hekima kuishinda elimu. Kwa hilo pia tunawashukuru viongozi wetu wa dini kwa hekima walioichukua kutokana na elimu waliyonayo katika suala hili zima.

Mungu ibariki Tanzania, Watu wake na Viongozi wake. Amin.

Samahani kama nimekosea popote.

Ndugu yenu,

Saleh Jaber.

28/08/2016

COME TO TANZANIA AND WITNESS ANNULAR SOLAR ECLIPSE, September 1, 2016

12065538_1196362963712903_3746619825889761272_n_630_450_c1

Tanzania Tourist Board wishes to welcome everyone from all over the world to come to Tanzania and witness the solar eclipse which according to astronomy experts Tanzania in particular Rujewa Area in Mbeya region located in Southern Highlands of Tanzania will be the best site for viewing this fascinating event where the sun’s disk will change to a ring.
This major astronomical event will occur on September 1 this year from 10:17am to 1:56pm, centered over Tanzania and is expected to attract eclipse chasers from around the world and across the country.

People in Tanzania will witness first-hand the sun go evening-dim at midday as more than 90% of the sun will be covered by the moon in a partial solar eclipse leaving the sun as a thin crescent. The annual eclipse will be seen as a thin bright ring on that day for hundreds of thousands of people living within a 100 kilometre band crossing Southern Tanzania from Congo into Katavi, Mbeya, Ruvuma, to Masasi and out to Mozambique. Experts say that the next eclipse in Tanzania is expected to occur after 15 years. So this is a great opportunity that one shouldn’t miss.

HOW TO GET THERE?

For UK citizens/residents who want to get visa to go to Tanzania to witness this astronomical event, please visit the Tanzania High Commission website link: http://tanzaniahighcomm.co.uk/ for more information on how to apply for a visa to Tanzania. For other countries, please check with the Tanzanian consulate in your country.

USEFUL LINKS BELOW:

Tanzania Tourism

Eclipse Tours

Mkuu Wa Mkoa Akabidhi Michoro Ya Makao Makuu Ya BAKWATA

RC. MAKONDA AKABIDHI MICHORO YA MAKAO MAKUU YA BAKWATA YATAKAYOGHARIMU SHILINGI BILIONI 5 NA MILIONI 80.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda amekabidhi ramani ya jengo la Makao Makuu BAKWATA linalotegemewa kuanza ujenzi wake mwaka huu na kukamilika ndani ya miezi 14 baada ya ujenzi kuanza. In shaa allah.

Mungu akuzidishie imani Mheshimiwa Makonda. Uongozi unaoacha Alama.


Taarifa Ya Maziko Ya Marehem Aboud Jumbe

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, ametoa taarifa rasmi ya Serikali kuhusu kifo cha Rais Mstaafu wa Zanzibar wa Awamu ya Pili, Mheshimiwa Alhaj Aboud Jumbe Mwinyi. 

Katika taarifa hiyo aliyoitoa kupitia vyombo vya habari, Alhaj Dk. Shein kwa masikitiko makubwa aliwaarifu wananchi kuwa leo tarehe 14 Agosti 2016, Mzee Alhaj Aboud Jumbe Mwinyi amefariki dunia, msiba ambao umetokea nyumbani kwake Mji Mwema, Kigamboni, Dar es Salaam.

Alhaj Dk. Shei alieleza kuwa Marehemu Mzee Aboud Jumbe ni Rais Mstaafu wa Zanzibar wa Awamu ya Pili, ambaye vile vile alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Marehemu Mzee Aboud Jumbe amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na umri wake. 

Kwa taarifa ya Alhaj Dk. Shein, maziko ya marehemu yatafanyika kesho tarehe 15 Agosti 2016 saa 7.00 mchana ambapo maiti yake itasaliwa katika Masjid Mshawar, Mwembeshauri na kuzikwa nyumbani kwake Migombani. 

Aidha, Alhaj Dk. Shein alieleza kuwa kufuatia mchango na juhudi kubwa ambazo Marehemu Mheshimiwa Aboud Jumbe Mwinyi alizichukua katika uhai wake kwa kuitumikia, kuiongoza na kuijenga Zanzibar pamoja na nafasi yake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Nchi yetu imekabiliwa na msiba mkubwa kwa kigfo cha kiongozi huyu mahiri”alieleza Alhaj Dk. Shein katika taarifa hiyo. 

Kutokana na msiba huo mkubwa Alhaj Dk. Shein alitangaza rasmi siku saba za maombolezo, kuanzia kesho tarehe 15 Agosti 2016 ambapo katika kipindi hicho chote bendera zote  zitapepea nusu mlingoti. 

Pamoja na hayo, Alhaj Dk. Shein alieleza kuwa utaratibu wa maziko utafuata wasia ambao mwenyewe marehemu aliutoa wakati wa uhai wake. 

“Tunaungana na Wanafamilia wote katika kipindi hiki kigumu cha msiba. Naomba kutumia nafasi hii kutoa mkono wa pole kwa wafiwa wote. 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie kauli thabit marehemu mzee wetu na amlaze pahala pema peponi, Amin. Inna lillahi wa inna ilayhi raajio’un.” Alieleza Alhaj Dk. Shein katika Taarifa hiyo.

Rais Wa Zamani Wa Zanzibar Afariki Dunia

aboud jumbe

Aliyekuwa Rais wa Zanzibar (1972-1984), Mzee Aboud Jumbe Mwinyi afariki dunia leo nyumbani kwake Kigamboni, Dar es Salaam.

Inasemekana maziko yanatarajiwa kuwa Zanzibar lakini bado haijathibitishwa.

Allah awape subra familia yake, na, amfanyie safari yake iwe nyepesi, amghufurie madhambi yake na ampe Jannat Firdous. Amin.

Serikali Ya Mwendo Kasi Ukingoni Mwa Kufikisha Mwaka Mmoja Tangu Kuwemo Madarakani

Ningependa kuchukua fursa hii kumpongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuleta kimbunga cha mabadiliko ambacho hakijawahi kutokea kwenye historia ya Tanzania tangu tupate Uhuru.

Sote tunajua maendeleo ya kila sekta ya nyanja zote za taifa hayaji kwa usiku mmoja kama nilivyosema kwenye makala yangu iliyopita kwa kumaanisha kuwa awamu moja peke yake haiwezi kuleta maendeleo tarajiwa ya kila sekta na kufikia ngazi ya kimataifa, hii huchukuwa muda na subra, lakini Mabadiliko yanaweza kutokea kwenye msimu mmoja au awamu moja kwa maana ya kuwa, inawezekana kwenye awamu moja kutokea mabadiliko ya Mfumo wa kuleta maendeleo ya kila sekta ya nyanja zote za taifa na kuwa kama ndiyo kitako au msingi wa maendeleo wa taifa zima kwa siku za usoni zijazo. Nimetumia neno kimbunga ni kutokana na kasi ya mabadiliko haya ya mfumo wa utendaji kazi unaotokea nchini kwetu hivi sasa kwenye sekta mbalimbali ambayo yanayosaidia kuichonga ile dira ya taifa ya mwaka 2025 na zaidi, kwa kutokomeza umaskini na kuwapa huduma bora za msingi na huduma stahiki kwa raia wa hali ya chini na raia wote kwa ujumla katika taifa letu adhim.

Rais wetu mheshimiwa John Pombe Magufuli ameamua kujikita kuleta maendeleo kwa kuleta Mapinduzi ya Viwanda ambayo mchakamchaka wake unastahili mapongezi kwake na majopo yake, na unastahili mapongezi kwa mawaziri wa sekta zote akiwamo Waziri Mkuu Kassim Majaaliwa kwa kazi kubwa wanayoifanya kwenye kila kona ya nchi na kushuka kwenye ngazi za chini kabisa kuhakikisha kuwa hakuna jiwe linaloachwa bila ya kupinduliwa-pinduliwa kuangaliwa wapi linaweza kuchongwa na wapi lifanyiwe marekebisho ya kwenda sambamba na maendeleo tarajiwa aliyoyadhamiria mheshimiwa rais ya miaka mitano, kumi na zaidi ijayo.

KUHAMA KWA MAKAO MAKUU

Nia ya serikali kuhamisha Makao Makuu yake Dodoma yalianza tangu miaka ya mwanzo ya sabini (1970’s), sote tulikuwa tunatarajia kuhama kwa makao makuu kutatokea ila ilibaki kuwa ni lini itatokea. Na tendo hili linaweza kuwa limewashtua baadhi ya watu likiwa kama ni jambo jipya kwao, lakini mahamisho ya makao makuu ya serikali si jambo geni, baadhi ya nchi za Afrika na nje ya Afrika zimehamisha makao makuu ya serikali zao kutoka mji mmoja kwenda mji mwingine kwasababu mbalimbali. Hongera mheshimiwa rais kwa kuchukuwa hatua ya kijasiri chini ya mwaka mmoja tangu kuanza kwa madaraka ya kuwa rais na kuhamisha makao makuu kwenda Dodoma. Baadhi ya watu wanaweza kuuliza nia na hoja ya kuhamia kwa ghafla na kwa haraka hivyo kwa kipindi cha miezi miwili tu tangu itangazwe nia rasmi ya kuhama kikamilifu kivitendo, lakini tunaamini kuwa kila penye nia pana njia na tunaomba kila la kheri, Mwenyezi Mungu haangalii matendo bali anaangalia nia.

FAIDA ZA KUHAMISHA MAKAO MAKUU

Tendo la serikali kuhamisha makao makuu Dodoma kimatendo, litapunguza gharama za kiutendaji kazi zaidi kuliko kama ilivyokuwa hivi sasa serikali ipo jijini Dar es Salaam lakini bunge lipo Dodoma, hivyo serikali kuhamisha makao makuu yote Dodoma, itasaidia kubana baadhi ya matumizi mengi ya kipesa, kiharakati na kimawasiliano.

Mji wa Dodoma upo katikati ya nchi ambapo ni rahisi wanaharakati, wabunge, mawaziri, wananchi na watendaji wengine wa serikali na wasio wa kiserikali kwa ujumla kufanya harakati zao na kuwasilisha kazi zao bila ya kusafiri mbali kama ilivyo hivi sasa, kwahiyo itakuwa nafuu kwa mtu anayetoka mfano kaskazini, kusini au magharibi mwa nchi kwenda Dodoma kuliko kuja Dar es Salaam, na watendaji kazi wa kiserikali wanaotoka Dodoma kufikia maeneo mengine ya nchi, ni rahisi na ni nafuu kwao kufika haraka miji mingine kutokana na Dodoma kuwa ipo katikati ya nchi yetu ya Tanzania.

Vilevile itasaidia kupunguza msongamano wa watu jijini Dar es Salaam kwa kiasi fulani, na hili ni jambo serikali la kuliangalia kwa siku za usoni kuwa kila mji wa Tanzania uwe na huduma zote za kutosheleza za kiserikali, na kila mji uwe na vivutio vya wananchi kupata kazi katika miji yao bila ya kuhamia mji mwingine eti kwasababu mji au miji yao haina fursa za kutosha. Hii ni kazi ya serikali kujipanga na kuwapelekea fursa hizo wananchi hasa kwa sasa ni wakati muwafaka wa mapinduzi ya viwanda kwa kuvitawanya viwanda kwenye miji mbalimbali (kwa kufuata miundo mbinu ya kisasa) na vilevile kuwashajiisha wananchi kuwa wajasiriamali katika miji yao ili waweze kuishi na kufanya kazi kwenye miji waliyokulia nayo, na hii isichukuliwe vibaya, kwa kuchukua hatua hizi ni bila ya kukiukwa katiba yetu ya nchi ambayo inampa mwananchi uhuru wa kuishi na kufanya kazi popote pale anapotaka kwa kuleta maendeleo yake yeye binafsi na maendeleo ya familia yake na jamii iliyomzunguka.

HASARA ZA KUHAMISHA MAKAO MAKUU BILA YA KUWA MAKINI

Sina shaka kuwa hatua ya rais kuhamishia makao makuu Dodoma ni ya kutimiza ndoto ya serikali ya kuhamia Dodoma tangu nia hiyo ilipotangazwa rasmi miaka ya mwanzo ya sabini (1970’s) na hongera sana kwa hilo na sina shaka kuwa serikali ipo makini kwa kuchukua hatua hiyo.

Pamoja na kutimiza ndoto ya kuhamishia makao makuu Dodoma, serikali isije ikajisahau na kuipa mgongo Chachu iliyotolewa na mpaka hivi sasa inayoendelea kutolewa na jiji la Dar es Salaam kwa kuleta maendeleo ya taifa hili na kufikia hapa lilipo. Dar es Salaam ndiyo mtoto, ndiyo mama, ndiyo baba na ndiyo mlezi, na maendeleo mengi yaliyopatikana katika nchi yetu yametokana na mkono na kinywa cha jiji la Dar es Salaam, kwa maana nyingine Dodoma itakuwa sasa ni bongo la taifa na Dar es Salaam itabaki na itaendelea kuwa ndiyo moyo wa taifa.

Serikali isije ikajisahau moja kwa moja kuacha kuendelea kuleta maendeleo ya jiji la Dar es Salaam na miji mingine kwa kulimbikiza mapato yote sehemu moja na kusahau sehemu nyingine, huku kunaweza kuleta mtikisiko wa kiuchumi nchini. Kwa kusema hivi, ni muhimu serikali iendelee kuleta maendeleo ya kisasa ya miundombinu na maendeleo mengine katika jiji la Dar es Salaam na miji mingine nchini ili kuleta maendeleo tarajiwa kwa wananchi kwa kutegemea ujasiriamali, viwanda na fursa mbalimbali nyinginezo. Kwa kufanya hivi kutasaidia nchi na miji ijitegemee yenyewe kiuchumi bila ya kutegemea sana maliasili za nchi, na hapa kunanipelekea kuzungumzia kuhusu Maliasili na Rasilimali za nchi yetu.

MALIASILI NA RASILIMALI ZA TAIFA

Kama mfano ilivyo nchi za wenzetu, mfano nchi ya Falme za Kiarabu (U.A.E.), ambayo makao makuu yake ni Abu Dhabi, lakini jiji la Dubai ndiyo inayojulikana duniani kote kwasababu imeshinda kwenye kujitegemea kiuchumi yenyewe kijasiriamali na kibiashara bila ya kutegemea sana maliasili za nchi kama mafuta (oil), gesi (gas), na kadhalika.

Sote tunajua sasa Mwenyezi Mungu katubariki na kaleta neema kubwa katika nchi yetu kwa kuwa na utajiri wa maliasili zikiwemo gesi, madini na maliasili nyingine mbalimbali ambazo nyingine zikiendelea kugunduliwa kila siku. Ikiwa tutakuwa tuna ubinafsi, si maanishi ubinafsi wa kujibinafsisha mtu mmoja, hapana, nazungumzia ubinafsi wa kizazi chetu kilichopo sasa hivi kwa kutumia vibaya maliasili hizi na kuanza kuchimba na kuchimbua kila tunapoona maliasili mpya zinapojitokeza na kuanza kuzitumia bila ya kujua kuwa hakuna kitu kisichokuwa na mwisho basi itakuwa tunawadhulumu vizazi vitakavyokuja miaka mia tano (500) na zaidi ijayo kuanzia hivi sasa, kwani wazee wetu wamesema, “Bandubandu humaliza gogo”. Kwa mfano, lazima tujue kuwa kila ujazo wa gesi iliyopo chini ya ardhi hata kama ikiwa ni trilioni ngapi, basi ipo siku itafikia mwisho wake, na maliasili za chini ya ardhi si kama miti ya kusema kuwa utakata mti leo utapanda mwingine kesho, ingekuwa hivyo basi kila nchi duniani ingekuwa na mafuta na gesi ya kutosha bila ya kutegemea mafuta au gesi ya mwenzie, na hata kama kutakuwa na teknolojia ya kutengenezea au kunakili gesi au mafuta, basi haitokuwa yenye kiwango cha asilia na gharama zake zitakuwa kubwa sana na za kupindukia. Si vibaya kuendelea kufanya utafiti wa maliasili na si vibaya kusimama kwa sasa, lakini siyo kila tunapoiona maliasili ya nchi tunaichimba na kuichimbua kwa manufaa ya kizazi cha sasa tu, hivyo itakuwa hatujatenda uadilifu kwa neema na zawadi hii tuliyopewa na Mwenyezi Mungu kwetu sisi na vizazi vyetu vijavyo.

Vilevile rasilimali za taifa, serikali ijitahidi kuzihodhi hizi rasilimali bila ya kuzibinafsisha ili ziweze kukidhi haja zake za kihuduma kwa raia wa Tanzania na huku ikiendelea kutengeneza rasilimali mpya mbalimbali kwa malengo mbalimbali na kuwapa fursa ya wawekezaji kujijengea rasilimali zao wenyewe binafsi zenye kunufaisha raia wa Tanzania; ningependa kusema “ni bora kukodisha kuliko kubinafsisha.” Vilevile hongera kwa kupigia breki mradi wa Chole, Mafia na kuuangalia kwa kina nini mustakbali wake kwa wakazi wa kijiji hicho Kiuchumi, Kiutamaduni na Kihistoria.

Huu ni ushauri wangu na samahani kama nimekosea popote. Tunamuombea Rais wetu John Pombe Magufuli, Mwenyezi Mungu amlinde, amzidishie afya, hikma na utawala bora. Amin.

 

Ndugu yenu,

 

Saleh Jaber

07/08/2016